Pages

Sunday, December 30, 2012

Tiba mbalimbali za Vitunguu Swaumu


MATUMIZI KATIKA NCHIMBALIMBALI
kitunguu ni kiambatanisho muhimu kidishi kimaendeleo katika sehemu nyingi ulimwenguni.
Zamani Egpta iliheshimiwa kuwa ya hadhi ya kimungu.

MAANDALIZI YA KITUNGUU SAUMU KIMADAWA
Kitunguu saumu na asali. Jaza chupa ya glasi na vitunguu saumu vilivyomenywa na
kukatwa katwa polepole mwaga katika asali ya kwamba inajaza nyufa katikati ya fundo ya

kitunguu. Weka glasi kwenye sehemu ya joto yenye c 20oc. Katika siku mbili hadi wiki nne,
asali itanyonya juisi ya kitunguu saumu na kitunguu hicho kitachechemea na kutoingiza

mwanga usichuje. Tumia katika muda wa miezi 3.
Kitunguu Saumu dawa ya kikohozi

Ponda kijiko cha chai cha kitunguu saumu katika kipimo hicho hicho cha sukari au asali.
Tumia mara moja k.mf. kwa kikohozi.
Kitunguu saumu mafuta. Weka g 200 za vitunguu vilivyokobolewa saga kitunguu saumu na

kuweka kwenye chombo cha glasi na ongeza mafuta ya kutosha (au vizuri mafuta ya chakula)

funga. Funga jagi kwa kubana vizuri, na weka ikae kwenye sehemu yenye joto kama C 20
kwa siku tatu. Tikisa mara chache kila siku. Halafu weka kwenye sehemu ya baridi, bila

kuchuja. Tumia katika muda wa mwezi mmoja.
Kitunguu saumu „tinkcha“. Loweka g 200 za vitunguu vilivyomenywa na kukatwakatwa
katika lita moja ya brandi au alikoholi 40-50%, kwa siku 14 kwenye C 20° katika chupa

yenye kufungwa vizuri bila kupitisha hewa. Tikisa chupa hiyo mara nyingi kwa siku. Chuja
vipande vya kitunguu saumu. Tinkcha inakaa muda wa mwaka.
MAPENDEKEZO YA MATUMIZI
Kula kitunguu saumu kibichi- hii ni bora.
Tumia katika kupika.

Kula vitunguu saumu vingi kuzuia magonjwa. Kitunguu saumu ni safi sana kwa mfano kuna
usemi kwamba, chakula chako kiwe ndiyo dawa yako, na dawa yako chakula chako. Hii ni
kweli tu, hata hivyo, kwa kitunguu saumu kibichi, kama ilivyo vitu vingi vyenye nguvu

vinaangamizwa katika kupikwa. Vitunguu saumu vibichi vinatia nguvu katika mfumo wa
kinga ya maradhi. Matumizi kawaida ya vitunguu saumu yameonyeshwa katika kupunguza
madhara ya magonjwa ya moyo, kiharusi, kansa, msukumo wa damu na homa ya mafua

makali (flu). Tunashauri kwa nguvu ya kuwa wanaoteseka kwa UKIMWI (AIDS) waweke
kitunguu saumu katika chakula chao cha kila siku, kupunguza nguvu ya magonjwa mengine.

Kwa sababu inafanya mara mbili, kwa matumizi ya nje na kwa ndani kama dawa ya kuua
wadudu, vitunguu saumu ni masaada wa kutibu magonjwa yote ya kuambukiza; Toifodi,
minyoo, bilhazia, malaria, damu yenye maambukizo na sumu n.k. Zaidi yake vitunguu saumu

vinaimarisha kumbukumbu, hupunguza shindikizo la damu na Homa, na vinafanya kazi
kupinga ugumu wa kuta za ateri (hardening of arteries). Vitunguu saumu pia vinapinga virusi
na dhidi ya kinyume cha mambo ya fangasi.


1.Majipu au uvimbe na chunjua.
Saga vitunguu saumu vibichi na funga vilivyopondwa kwenye sehemu ya jipu, uvimbe au
Chunjua mara mbili kwa siku na gandamiza. Anza matibabu haya mapema iwezekanavyo.

2. Amiba.
Katakata vitunguu saumu sawasawa vipande vidogo na chukua kijiko kikubwa 1 pamoja na
Chai mara tatu kwa siku (usitafune, kusaidia kupinga kutoa harufu mdomoni). Endelea na
Matibabu haya kwa siku 5. I (H-M Hirt) aliponywa mwenyewe toka Amiba kuharisha
damu kwa Tiba hii.

3. Malaria.
Katakata vitunguu saumu sawasawa. Meza kijiko kimoja cha vitunguu hivi mara tatu kwa
Siku na kunywa lita 2 za limao glasi ya chai kwa siku. Endelea na tiba hii kwa siku 5.
Angalia pia ukurasa wa 8 kwa ajili ya malaria.

4. Kisukari, shindikizo la damu, kinga ya ugumu wa kuta za arteri (hardening of the
arteries).
Kula vitunguu saumu kwa wingi, vitunguu saumu na vitunguu vinapunguza sukari katika
damu na kusawazisha damu ya cholesteroli, na shindikizo la damu. Badala yake chukua
matone 20 ya vitunguu tinkcha mara 3 kwa siku, basi hii ni pungufu ifuatayo:

5. Kikohozi, homa, sinusitis na kuvimba koo.

a) Kula klovu ya vitunguu saumu mara tatu kwa siku.

b) Chukua kijiko cha chai cha kitunguu saumu asali kila masaa machache.

c) Watoto wanaweza kutumia kijiko cha chai cha kitunguu saumu
mchanganyiko kila baada ya masaa machache.

d) Chukua kijiko cha chai cha kitunguu saumu mafuta mara 6 kwa siku.

6. Kandika.
Chukua kijiko cha chai cha kitunguu saumu au kitunguu saumu yenye asali, kila masaa
machache. Weka mdomoni kwa muda mrefu iwezekanavyo.

7. Fangasi inayoambukiza pamoja na ugonjwa wa ukungu kwenye vidole vya miguu.
Funga sehemu zilizoathirika kwa juisi ya vitunguu saumu vibichi vilivyopondwa au
mafuta.

8. Homa ya matumbo na maambukizo mengine.
Kama itatokea homa ya matumbo, bacillary, kuharisha damu, kifua kikuu, kipindupindu,
trypanosomiasis (ugonjwa wa kusinzia): Siku zote ongeza kitunguu saumu kwa tiba ya
kawaida.

9. Kinga ya mishipa ya damu.
Kitunguu saumu siku zote kinafanya damu kuwa laini na kukinga kutengeneza damu
kuganda ambayo inasababisha shida ya thrombosis. Hii ni muhimu kwa wagonjwa
wanaolala kitandani kwa muda mrefu.

10. Kuota meno utotoni.
Futa ufizi kwa fundo la kitunguu saumu.

MADHARA YAKE
Kitunguu saumu kinaweza kukera ngozi hasa baada ya kutumia kwa muda mrefu. Epuka
kuhusisha kwenye macho.

0 comments:

Post a Comment